![](https://scontent-lga1-1.xx.fbcdn.net/hphotos-xtf1/v/t1.0-9/11390291_1244999145514501_1616281789149572148_n.png?oh=3b1636dfd576524d08cd33860b6bc5f8&oe=562E21DC)
Waziri Mkuu wa Tanzania Mhe. Mizengo Pinda ameingia rasmi katika kinyang'anyiro cha kuwania urais kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), ambapo hii leo amechukua fomu za kuwania urais katika makao makuu ya chama hicho Mkoani Dodoma.
Akiongea mara baada ya kuchukua fomu za kuwania urais, Mhe. Pinda amesema iwapo atateuliwa kuwania urais na chama chake atatekeleza Ilani ya CCM, pamoja na mpango wa maendeleo wa miaka mitano wa kuondoa umasikini wa hali ya chini kabisa.