MSANII RAY C ALIA KWA UCHUNGU BAADA YA KUNYIMWA DAWA YA METHADONE YA MADAWA YA KULEVYA,VIDEO IKO HAPA


Rehema Chalamila aka Ray C amejikuta akishindwa kujizuia kulia baada ya kunyimwa dawa ya Methadone ambayo amekuwa akiitumia kwa miaka miwili sasa ili kumsaidia kuondokana na addiction ya madawa ya kulevya.


Ray C amepost video kwenye Instagram ambazo kwa zinaendelea kusambaa kwenye mtandao huo akilia kwa uchungu.

“Nashindwa kuvumilia,” anasikika akisema. “Mpaka sasa nipo hapa kitengo cha madawa na sijapewa dawa, kwa sababu nilipost ile post nyingine wamenifanyia makusudi. Sasa mimi nikikosa madawa wanataka nirudi kwenye kuvuta unga,” amehoji muimbaji huyo.

Ray C aliendelea kudai kuwa mwili unamuuma pamoja na mifupa huku akishindwa kujua afanye nini ili kukabiliana na hali hiyo ambayo amedai inamtesa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post