Makubwa HAYA>>MUME NA MKE WAMENUNUA NYANYA SUPERMARKET......WALICHOKUTANA NACHO BAADA YA KUFUNGUA NI STORI.....

lizad

Pata picha unaingia zako supermarket, unanunua mahitaji mbalimbali ya jikoni na unabaki na hesabu moja tu nyepesi kwamba ukifika home kazi yako ni kupika, alafu unakuja kufungua unakutana na vitu vya ajabu.

Muhammad Hussain na mkewe Sanam wanaishi Birmingham, Uingereza.. Walitoka zao Supermarket na vitu mbalimbali walivyonunua, kuja kuingia jikoni kwa ajili ya kuandaa chakula mwanamke huyo akakuta ndani ya kopo la nyanya kuna mjusi aliyekufa.
lizad2
Pamoja na kupeleka malalamiko yao kwa uongozi wa Supermarket hiyo inayoitwa Masala Bazaar waliombwa radhi kwa kitendo kilichotokea, wakaahidiwa kwamba kutafanyika uchunguzi jinsi gani imetokea mpaka mjusi huyo kaingia ndani ya kopo hilo ambalo ni ka nyanya ambazo zimesindikwa toka Italy.
lizard4
“Mke wangu alikuwa jikoni anaandaa chakula cha mchana, nikasikia anapiga kelele.. kwenda nikakuta ndani ya kopo hilo la nyanya kuna mjusi aliyekufa“– Muhammad Hussain.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post