Makubwa Haya!! JAMAA AFATUNA VIPANDE VYA COMPYUTA YAKE.....KILICHOFUATA NI STORI.....




Kuna sababu nyingi zinazopelekea mtu kupoteza ushahidi wake lakini kuna wengine hufikia hata kuhatarisha maisha yao ili tu waweze kutimiza ndoto zao kama ambavyo imetokea kwa kijana huyu.


Mwanaume mmoja amepoteza maisha baada ya kula vifaa vya kompyuta yake aliyokuwa akiitumia ili kupoteza ushahidi wakati akiwa anatafutwa na polisi huko Russia.


Polisi walisema mtu huyo aliamua kufanya hivyo ili kukosa ushahidi wa kumfunga wakati askari hao walipofika nyumbani wake kwa ajili ya kufanya uchunguzi.


Wakati wakifanya uchunguzi alianza kula baadhi ya vifaa hivyo huku afisa mmoja wa polisi akijeruhiwa wakati akimzuia mtu huyo kutekeleza maamuzi yake na alipoteza maisha kabla ya kupatiwa matibabu.


Hata hivyo askari hao hawakuweka wazi walikua wakimfanyia uchunguzi kuhusu tuhuma gani.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post