Hatari!! KUNDI LA KIHALIFU LAIBUKA,WANANCHI WAPIGWA NONDO NA MAPANGA

Habari kutoka  wilaya ya Songea mkoani Ruvuma zinasema kuwa kumeibuka kikundi cha kihalifu cha wapiga nondo na wakata mapanga ambao pia wamekuwa  wakipora pikipiki na mali mbalimbali.

Hata hivyo jeshi la polisi mkoani Ruvuma limefanikiwa kuwakamata watuhumiwa tisa wa kikundi hicho na mali kadhaa za wizi.


Kamanda wa polisi wa mkoa wa Ruvuma ACP Mihayo Msikhela amesema mali kadhaa za wizi zimekamatwa zikiwemo simu,Deki na Tv.
 
Kamanda Msikhela amesema kuwa wahalifu hao wamekuwa wakitumia nondo,mapanga kisha kuvamia watu na kufanya uporaji wa mali zikiwemo pikipiki na kwamba watu tisa wanashikiliwa kwa uhalifu huo.
 
Via>>ITV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post