RONALDO ATAONDOKA MADRID,JE ATAVUA JEZI KWA DILI LA MIL 280 ZA PSG?

C Ronaldo II
Ziliwahi kukaa story kwenye magazeti na mitandao mikubwa ya habari duniani kwamba staa wa soka, mreno Cristiano Ronaldo atarudi kuichezea klabu yake ya zamani, Man United.. ikapita muda hilo halikutokea.


Imekuja nyingine, tayari imeanza kuchukua headlines kwamba Ronaldo ataondoka Madrid, safari yake inakuwa kwenda wapi? Mezani dau limewekawa kiasi gani? Majibu niko nayo tayari.
C Ronaldo 
“PSG offer €125 for Ronaldo”—kichwa cha habari chenye wino mzito kwenye gazeti la michezo la Madrid, Hispania… story ndani ni kwamba Klabu ya PSG ya Ufaransa wametangaza dau la Euro Mil. 125 (sawa na kama Bil. 280 hivi) kwa ajili ya kumvuta staa huyo ajiunge na kikosi chao japo mwenyewe bado hajatolea majibu kuhusu ishu hiyo.. tetesi nyingi za ishu za soka mara nyingi zinakuwa na chembe chembe za ukweli hivi, na hii je?

Story nyingine inasema staa huyo ni kama hayuko tayari kuondoka Madrid mpaka mkataba wake utakavyoisha msimu wa 2017/18.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527