MATOKEO MCHEZO KATI YA YANGA Vs AZAM ,SASA AZAM HATUA MOJA MBELE MICHUANO YA KIMATAIFA

AzamFC3-660x280

Kwa mara nyingine Kikosi cha timu ya Simba wanakosa kushiriki wa michuano ya kimataifa kwa msimu wa pili mfululizo baada ya Azam kufanikiwa kushinda dhidi ya mabingwa wa ligi kuu Yanga kwenye uwanja wa Taifa.

Azam wamejihakikishia nafasi hiyo ya kimataifa baada ya ushindi wa mabao 2-1 walioupata Azam dhidi ya mabingwa wapya wa ligi kuu msimu huu Yanga.


Kwa ushindi wa Azam ambao walikuwa wakichuana na Simba kusaka nafasi ya pili, sasa imefikisha pointi 48 ambazo haziwezi kufikiwa na Simba wenye pointi 44 ambao wamebakiza mchezo mmoja na hata wakishinda watakuwa wamefikisha pointi 47.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post