JINSI RAIS WA MSUMBIJI ALIVYOWASILI NCHINI TANZANIA


Rais wa Msumbiji Mhe Filipe Nyussi amewasili nchini Tanzania kuanza ziara yake ya kikazi ikiwa ni ziara yake ya kwanza kuifanya hapa nchini tangu achaguliwe kuwa rais wa nchi hiyo.



Rais wa Msumbiji Filipe Jasinto Nyussi amepokelewa na mwenyeji wake rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta Jakaya Mrisho Kikwete ambapo baada ya utambulisho kwa baadhi ya viongozi waliojitokeza kumpokea rais huyo nyimbo za taifa zikiimbwa.

Nyimbo hizo ziliambatana na upigwaji wa mizinga kisha rais Nyussi akapata nafasi ya kukagua gwaride maalum lililoandaliwa kwaajili yake huku shamrashamra za shangwe na burudani ya ngoma za asili zikionesha ukarimu wa watanzania.
Akiwa Tanzania rais Nyusi atazungumza kwa faragha na mwenyeji wake rais Jakaya Mrisho Kikwete, kuongea na wafanyabiasha wa Msumbiji waishio hapa nchini ambapo tarehe 18 ataendelea na ziara yake visiwani Zanzibar kisha tarehe 19 rais Jasinto atahitimisha ziara yake mjini Dodoma kwa kuhutubia bunge la bajeti linaloendelea mjini humo.
Via>>Itv

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post