BASI LA SUPER FEO LATUMBUKIA MTONI LAUA WATU WATATU NA KUJERUHI 28


Watu 3 wamekufa papo hapo na wengine 28 kujeruhiwa baada ya basi la kampuni ya Super Feo walilokuwa wakisafiria kutoka jijini Mbeya kwenda Songea mkoani Ruvuma kupinduka na kutumbukia mtoni katika kijiji cha Shamwenga kata ya Inyara wilayani Mbeya.
 

Ajali hiyo imetokea baada ya basi la kampuni ya Super Feo likiwa kwenye mwendo mkali kujaribu kulipita lori lililokuwa mbele yake, lakini kabla halijafanikiwa kulipita kwa mbele likatokea lori la mafuta, hali ambayo ikasababisha dereva wa basi kulikwepa kwa upande wa kulia, lakini akashindwa kulimudu na ndipo lilipopoteza mwelekeo na kutumbukia mtoni.
 
 
 
Daktari wa zamu katika hospitali ya rufaa Mbeya, Dk Lathan Mwakyusa amethibitisha kupokea miili ya watu watatu pamoja na majeruhi 28 wanaotokana na ajali hiyo.
 
Amesema waliolazwa ni wanne walioruhusiwa ni 24.
 
Kwa upande wake afisa mfawidhi wa Sumatra mkoa wa Mbeya, Denis Daudi amesikitishwa na ajali hiyo na kuwataka madereva kuongeza umakini wawapo barabarani ili kuepusha ajali zinazoweza kuzuilika.

Via>>ITV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527