Wahamiaji haramu saba kutoka nchi ya Somalia na Ethiopia wamekamatwa
mkoani Shinyanga wakiwa kwenye magari ya abiria kuelekea jijini Dar es salaam
na wilayani Kahama na baadaye kusafirishwa kwenda nchini Afrika Kusini.
Kamanda wa polisi mkoa
wa Shinyanga Justus Kamugisha amesema wahamiaji hao haramu wamekamatwa Aprili
26 na 27 mwaka huu katika nyakati mbili tofauti kufuatia msako na doria ya askari
wa jeshi la polisi.
Miongoni mwa waliowakamatwa wamo raia wanne wa Somalia ambao walikamatwa katika
kijiji cha Isela kata ya Samuye wilaya ya Shinyanga Vijijini wakiwa kwenye basi
dogo lenye namba za usajili T.866 DCQ fuso inayojulikana kwa jina la Tiger Bus.
Amewataja wahamiaji hao kuwa Dasent Taraky(15),Abuu Undure(30) Tagasa
Aebete(25) na Izrael Abunne(18) ambao walikuwa wakisafiri kutoka Mwanza
kuelekea Kahama .
Amesema raia hao wa kigeni walikuwa wakisafirishwa na Issa
Juma(21) na Maulid Juma (19) wote wa kazi wa Majengo wilayani Kahama ambao pia
wanashikiliwa na jeshi la polisi.
Amesema kundi la pili la wahamiaji waliokamatwa ni la raia
watatu kutoka nchi ya Ethiopia ambao walikamatwa Aprili katika stendi ya mabasi
ya Ibinzamata mjini Shinyanga wakitokea mkoani Mwanza kuelekea jijini Dar es
salaam katika basi lenye namba za usajili T.974 YOUTONG mali ya kampuni ya
Master City na walikuwa wanasafirishwa na watu ambao hawajafahamika.
Kamanda Kamugisha amewataja wahamiaji hao kuwa ni Fireza
Wehmebo(19),Dawiti Esatu(18) na Dagafa Geje(18) wote wakazi wa South Hawasa
nchini Ethiopia.
Kamanda Kamugisha amewataka watanzania kuacha tabia ya kujihusisha na vitendo vya kuwahifadhi na kuwasafirisha watu hao na atakayekamatwa atafikishwa mahakamani na sheria itachukua mkondo wake.
Kamanda Kamugisha amewataka watanzania kuacha tabia ya kujihusisha na vitendo vya kuwahifadhi na kuwasafirisha watu hao na atakayekamatwa atafikishwa mahakamani na sheria itachukua mkondo wake.
Kwa upande wao watanzania wanaotuhumiwa kuwasafirisha wahamiaji hao haramu wamesema
wao wametumwa kuwachukua watu hao mkoani Mwanza na kuwafikisha katika
mji wa Kahama ambapo mtu mwingine atawachukua na kuwapeleka Afrika Kusini kupitia Dar es salaam huku wahamiaji hao haramu wakidai kuwa
wanasafiri kwenda Afrika Kusini kutafuta maisha mazuri kwa kua nchini
kwao hali ya maisha ni duni.
Na Kadama Malunde-Shinyanga