NAY WA MITEGO AELEZA KWANINI ALINUNUA SANAMU YA SHETANI


Nay wa Mitego ni mtu wa maamuzi na mapenzi tofauti na wengine. Ndio maana ukiingia ndani kwake utakutana na sanamu isiyo ya kawaida – ni sanamu ya shetani!

Rapper huyo ameiambia Bongo5 kuwa sanamu hiyo ni moja ya vitu anavyovipenda zaidi ndani mwake.

“Mimi naipenda na niliinunua hela nyingi tu, ni dola elfu tatu,” amesema Nay.

“Nilitokea tu kuipenda, ni moja kati ya vitu muhimu ninavyovipenda ndani ya nyumba yangu. Kuna sehemu niliinunua sio Tanzania. “Mimi nilitokea kukipenda yaani naipenda sana tena sana na hata ukiingia ndani kwangu utaanza kuiona hiyo,” amesisitiza rapper huyo. 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post