ANGALIA PICHA- SHEREHE ZA MAADHIMISHO YA MIAKA 51 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR

 
 Rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akipunga mkono kuwasalimia wananchi wakati alipokuwa akiwasili kwenye Uwanja wa Uhuru, Jijini Dar es salaam, leo kwa ajili ya kuhudhuria Sherehe za Maadhimisho ya Miaka 51 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Kushoto ni Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Davis Mwamunyange

 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiwa na baadhi ya Viongozi wenzake wa Serikali, wakisimama kutoa heshima wakati ikipigwa mizinga 21, uwanjani hapo.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, akikagua gwaride la heshima, wakati wa sherehe za Maadhimisho ya miaka 51 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar zilizofanyika kwenye Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam, leo.

*************
Rais Jakaya Kikwete ambaye pia amiri Jeshi mkuu wa majeshi ya ulinzi na usalama amewaongoza maelfu ya watanzania katika sherehe za maadhimisho ya miaka 51 ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar yaliyofanyika katika uwanja wa uhuru jijini dar es salaam.


Katika maadhimisho hayo yaliyohudhuriwa na maelfu ya watanzania,mabalozi,viongozi wa serikali na vyama vya siasa,Rais Kikwete aliingia uwanjani hapo akiwa katika gari la wazi akiwa  na mkuu wa majeshi ya ulinzi Janerali Davis Mwamunyange na kuzunguka uwanja wa uhuru akiwapungia mkono watanzania.


 
Rais kikwete kisha alipanda katika jukwaa maalum lililoandaliwa na kisha mizinga 21 ilipigwa pamoja na wimbo wa taifa na hatimaye alikagua vikosi mbalimbali vya majeshi ya ulinzi kabla ya kupanda katika jukwaa kuu nakusalimiana  na viongozi waandamizi wa serikali ya jamhuri ya muungano na serikali ya mapinduzi ya Zanzibar.


 
Aidha vikosi mbalimbali vya majeshi ya ulinzi vilipita mbele ya jukwaa kuu na kuonyesha ukakamavu na utayari wa kukabiliana na changamoto mbalimbali zitakazojitokeza.


 
Wakizungumza na waandishi wa habari baadhi ya viongozi wastaafu walioshuhudia mkataba wa muungano  mwaka 1964 akiwemo Spika Mstaafu Pius Msekwa wamewataka vijana kuuenzi muungano Tanzania na Zanzibar huo hususani katika kipindi hiki taifa linapokabiliwa na uchaguzi mkuu pamoja na mchakato wa katiba pendekezwa.


 
Burudani mbalimbali zilipamba sherehe hizo ikiwemo vijana na halaiki kuchora maumbo na kuandika maeneo mbalimbali,huku kikosi cha vijana wengine wakionyesha ukakamavu wa kupita kwenye moto pamoja na kutambaa katika kamba,pamoja na ngoma za asili zilikuwa kivutio kikubwa uwanjani hapo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527