MAFURIKO YAUA WATU 14

Watu 14 wameuawa kwenye mafuriko nchini Madagascar ambapo pia wengine 20,000 wamelazimika kuhama makwao.


Mafuriko hayo yaliukumba mji mkuu Antananarivo na maeneo yaliyo karibu.

Utawala unasema kuwa mvua nyingi siku zijazo huenda ikasababisha madhara zaidi.

Mvua kubwa imenyesha nchini humo kwa takriban wiki mbili.

Mwezi uliopita kimbunga Chedza kiliwaua watu 80 nchini Madagascar.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527