KIKONGWE WA SHINYANGA AFUNGUKA MAZITO , AITAKA SERIKALI KUACHA KUKURUPUKA NA WAPIGA RAMLI

Serikali imeshauriwa kutekeleza kwa uangalifu mkubwa adhima yake ya kupambana na waganga wa jadi wanaojihusisha na upigaji ramli zinazodaiwa ni chanzo cha mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albinism) kwa vile hatua hiyo inaweza kusababisha madhara makubwa kwa taifa.
 
Ushauri huo umetolewa na mmoja wa wazee maarufu mjini Shinyanga, Iddi Juma ambapo amesema serikali haipaswi kukurupuka katika kushughulikia suala la waganga wa jadi kwa vile baadhi yao wana umuhimu mkubwa kwa jamii na wamekuwepo nchini tangu enzi na enzi.
 "Hivi kweli kuna tiba yoyote ya majini au mapepo machafu katika hospitali zetu nchini? wanaopatwa na matatizo haya mara nyingi tunaona wanakimbizwa kwa waganga wa jadi, ndiyo wataalamu wa kuyatibu, na huko ni lazima mganga afanye mambo yake ili kubaini yametokea wapi, sasa tukiwakamata wenye matatizo haya watatibiwa wapi?" alihoji Juma.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527