KIKONGWE WA SHINYANGA AFUNGUKA MAZITO , AITAKA SERIKALI KUACHA KUKURUPUKA NA WAPIGA RAMLI
Saturday, January 31, 2015
Serikali
imeshauriwa kutekeleza kwa uangalifu mkubwa adhima yake ya kupambana na
waganga wa jadi wanaojihusisha na upigaji ramli zinazodaiwa ni chanzo
cha mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi (albinism) kwa vile hatua hiyo
inaweza kusababisha madhara makubwa kwa taifa.
Ushauri
huo umetolewa na mmoja wa wazee maarufu mjini Shinyanga, Iddi Juma ambapo amesema serikali haipaswi
kukurupuka katika kushughulikia suala la waganga wa jadi kwa vile baadhi
yao wana umuhimu mkubwa kwa jamii na wamekuwepo nchini tangu enzi na
enzi.
"Hivi
kweli kuna tiba yoyote ya majini au mapepo machafu katika hospitali
zetu nchini? wanaopatwa na matatizo haya mara nyingi tunaona
wanakimbizwa kwa waganga wa jadi, ndiyo wataalamu wa kuyatibu, na huko
ni lazima mganga afanye mambo yake ili kubaini yametokea wapi, sasa
tukiwakamata wenye matatizo haya watatibiwa wapi?" alihoji Juma.
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin