Jumla ya Watoto 200 waliozaliwa mwaka uliopita(2014), ambao wazazi wao walipimwa na kukutwa na maambukizi
ya virusi vya ukimwi (VVU), Mkoani Shinyanga, watoto 198 kati yao ndiyo
walionusurika na maambukizi ya ugonjwa huo, baada ya kuzaliwa salama, huku
wawili wakibainika kuwa wameathirika.
Mganga mkuu wa mkoa wa Shinyanga Dkt Ntuli Kapologwe
ameyasema hayo wakati akizungumza na Malunde1 blog, kuhusiana na mikakati ya mkoa kupunguza
maambukizi mapya ya (VVU),kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Dkta Kapologwe
amesema mwaka 2014) jumla ya akina mama wajawazito 200, waliobainika kuwa na
maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU),waliofika kliniki na kupimwa katika
Zahanati, Vituo vya afya, hospitali za wilaya na mkoa, walianza kupatiwa dawa
za kuzuia maambukizi hayo mapya kwenda kwa mtoto, ambapo wazazi 198, walijifungua
watoto wasiokuwa na maambukizi ya VVU.
“Baada ya akina mama wajawazito
hao kupimwa na kubainika kuwa wana maambukizi ya virusi vya ukimwi (VVU),
ndipo wakaanza kupatiwa dawa mara moja, ili kuzuia maambukizi mapya kwenda kwa
mtoto, ambapo akina mama tuliwapa dawa inayoitwa TLE,(TEMOFOVIR LAMIVUDINE EFAVERENZ)”,alifafanua Dkt Kapologwe.
"Watoto pia tuliwapatia dawa inayoitwa Niverapine, ambayo nayo inazuia
mtoto asipate maambukizi hayo mapya ya (VVU),kutoka kwa mama",aliongeza Dkt Kapologwe.
Amesema watoto hao wamenusurika kupata VVU kutokana na akina mama hao kujitokeza kupima afya zao na kufuata masharti na kuongeza kuwa
changamoto kubwa iliyopo katika mkoa wa Shinyanga ni akina mama wengi
kutofika kliniki na wengine kukimbilia kwa wakunga wa jadi na
kujifungulia majumbani hali ambayo inachangia vifo vingi vya watoto.
|
Social Plugin