Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Justus Kamugisha |
Askari wa jeshi la wananchi Tanzania MT.88596 Benard
Mdika(29) wa kambi ya Old Shinyanga
amefariki dunia papo hapo baada ya pikipiki aliyokuwa akisafiria
kugongwa na gari katika barabara ya Old Shinyanga maeneo ya shule ya sekondari
KOM iliyopo katika kata ya Lubaga
manispaa ya Shinyanga.
Kwa mujibu wa kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Justus
Kamugisha tukio hilo limetokea Januari 15,2015 saa 3:40 usiku baada ya gari
lisilofahamika namba za usajili,dereva wala mmiliki wake liligonga pikipiki
yenye namba za usajili T.984 BGH aina ya sunlg ikiendeshwa na askari huyo.
Kamanda Kamugisha alisema askari huyo kutoka kambi ya jeshi ya Old Shinyanga
aliyekuwa anaendesha pikipiki hiyo alifariki dunia papo hapo huku abiria wake
ambaye pia ni askari wa jeshi la wananchi MT 88789 PTE Nicholaus Donald(29) mkazi wa Old Shinyanga akijehuhiwa
katika sehemu mbalimbali za mwili wake.
Kamanda huyo alisema
Nicholaus Donald aliumia usoni na
kichwani na amelazwa katika hospitali ya rufaa ya mkoa wa Shinyanga na hali
yake inaendelea vizuri.
Alisema chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi wa dereva wa
gari na jeshi la polisi linaendelea na juhudi za kulitafuta gari husika na
dereva.
Na Kadama Malunde-Shinyanga