MUME AUA MKE KWA SHOKA,KISA KWANINI KAPIKA NYAMA YA NG'OMBE BADALA YA KUKU SIKUKUU YA KRISMAS

 

Kama ulifanikiwa kuisherehekea Christmas ya mwaka huu 2014 kwa amani basi ni heri kwako, kumbe wakati wengine wakisherekea kwa amani Sikukuu hii kubwa ya mwaka kuna sehemu ambazo hakukuwa na heri yoyote siku hiyo.

Story hii ya kusikitisha inatoka Kenya ambapo jamaa mmoja Daniel Imonje, alimpiga mke wake kwa shoka mpaka kufariki, majirani walioshuhudia wakisema eti kisa ilikuwa ni kitendo cha mke wake huyo kutomuandalia mume wake nyama ya kuku siku ya Christmas, badala yake akaandaa rosti ya nyama ya ng’ombe.

Ni wengi waliolaani  kitendo hicho kilichotokea Kijiji cha Shanderema, Kenya na mashuhuda wamesema Daniel alifanya unyama huo akiwa amelewa.

Mtuhumiwa anashikiliwa katika kituo cha Polisi cha Kakamega baada ya kufanya mauaji hayo kwa ajili ya uchunguzi.

Mpenzi Msomaji wetu,Tunapenda kukutumia Habari zetu zote mara tu Tunapoziweka Mtandaoni.Kujiunga nasi Bonyeza Hapa "HABARI" VITUKO "MAPENZI"MAGAZETI,UDAKU>
Endapo una Habari,Picha,Video,Tangazo au Tatizo Lolote wasiliana nasi kwa namba  +255 688 405 951

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527