JINSI RAIS KIKWETE ALIVYOWASILI NCHINI AKITOKEA MAREKANI KUTIBIWA TEZI DUME

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Prof. Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) akiongea na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa J.K. Nyerere jijini Dar es Salaam leo,mara baada ya kuwasili nchini akitokea nchini Marekani kwenye Matibabu.

Rais Jakaya Kikwete amewataka Watanzania kujenga utaratibu wa kupima afya zao mara kwa mara, ili waweze kutibiwa wanapogunduliwa na maradhi.


Rais Kikwete ametoa changamoto hiyo alipozungumza na wananchi na waandishi wa habari katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere,waliokwenda kumpokea wakati anarejea kutoka Marekani alikowenda kwa matibabu ya tezi dume.

Amewahakikishia watanzania kuwa  afya yake imeimarika baada ya matibabu hayo na kuwataka  watanzania kuwa na amani nakuendelea kumuombea.

Amewashukuru watanzania waliomtumia salamu za kumfariji na kumtakia afya njema alipokuwa katika hospitali ya Johns Hopkins iliyoko  mji wa Baltimore, jimbo la Maryland  nchini Marekani.

Amesema sasa ana afya njema na amani moyoni kuliko alivyokuwa awali kwani hakujua ambacho kingetokea, kwani ali amini kuwa maradhi aliyokuwa nayo ni saratani kama ilivyobainika.


BONYEZA HAPA UJIUNGE NASI TUKUTUMIE HABARI ZETU MARA TU TUNAPOZIWEKA 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527