JAMAA AJINYONGA,AKUTWA NA UJUMBE " NAWAACHIA DUNIA YENU MUISHI MIAKA 110"

shambani

Mwanamme mmoja ambaye hakujulikana jina, amekutwa akiwa amejinyonga ndani ya kibanda shambani huku akiwa na karatasi iliyoandikwa ujumbe “Nawaachia dunia yenu muishi miaka 110”


Mwenyekiti wa Kijiji cha Kibiki, Ally Hussein alisema  mwanamume  huyo amekutwa saa mbili usiku akiwa amefariki na hivyo kutoa taarifa katika Kituo cha Polisi Chalinze.

Alisema askari walifika na kuukuta mwili wa marehemu ukiwa umefungwa kamba ya katani na alipopekuliwa alikutwa mfukoni na karatasi yenye maandishi hayo.

Kaimu Kamanda wa Polisi Pwani, Mrakibu msaidizi, Athumani Mwambalaswa amethibitisha tukio hilo na kusema mwili wa marehemu ulichukuliwa na kuifadhiwa Kituo cha Afya Chalinze kusubiri uchunguzi wa daktari.


Hata hivyo, alisema bado haijafahamika mtu huyo ni mwenyeji wa kijiji kipi kwani hapo Kibiki hakuweza kutambulika na jitihada za kutafuta ndugu zake katika vijiji vya jirani zinafanyika. Chanzo cha kujinyonga bado hakijajulikana.

TAFADHALI BOFYA HAPA U LIKE PAGE YETU TUKUTUMIE "HABARI" MOJA KWA MOJA KILA ZINAPOTOKEA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527