HOUSE GIRL WA MFANYAKAZI WA BENKI AUAWA KWA KUNYONGWA SHINYANGA CHUMBANI KWAKE


Kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga SACP Justus Kamugisha
Matukio ya mauaji yameendelea kuukumba mkoa wa Shinyanga ambapo huko katika mtaa wa Majengo Mapya Mjini Shinyanga, mfanyakazi wa ndani, Eliwaza Damiano (15)  ameuawa kwa kunyongwa kwa kutumia nguo aina ya khanga katika chumba chake cha kulala katika nyumba ya muajiri wake.

Tukio hilo limetokea jana majira ya saa moja usiku ambapo mfanyakazi huyo wa ndani wa alikutwa ameuawa  kwa kunyongwa na watu wasiojulikana ambao pia waliiba kompyuta mpakato(Laptop) moja,mkoba wa mkononi ukiwa na shilingi 20,000/= kisha kutokomea kusikojulikana.

Jeshi la polisi mkoani Shinyanga limethibitisha kutokea kwa tukio hilo,na kamanda wa polisi Justus Kamugisha amesema mwili wa marehemu uligunduliwa na muajiri wake Elizabeth Joseph (38) ambaye ni mfanyakazi wa benki ya CRDB tawi la Shinyanga mjini ambaye baada ya kutoka kazini alimkuta mfanyakazi wake ameuawa.

Kamanda Kamugisha ameongeza kuwa katika uchunguzi wa awali umeonyesha kuwa marehemu aliuawa kwa kunyongwa na khanga shingoni na watu wasiojulikana.

Na Kadama Malunde-Malunde1 blog-Shinyanga

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post