MWANAFUNZI ATUMBUKIA KWENYE SHIMO LA MAJI NA KUFARIKI DUNIA HUKO MBEYA

Mwanafunzi wa shule ya Sekondari Nandanga wa kidato cha kwanza Lukas Msukwa amefariki dunia baada ya kutumbukia katika shimo la Maji lililochimbwa na watengeneza barabara ya Mpemba hadi Wilayani Ileje, Mkoani Mbeya.
 
Tukio hilo limetokea juzi majira ya saa saba mchana katika Kijiji cha Nandanga, wilaya ya Momba ambapo inadaiwa kuwa chanzo cha tukio hilo ni baada ya marehemu kuteleza na kutumbukia katika shimo hilo lenye urefu wa kina kati ya futi 20 na zaidi ambalo lilikuwa na maji.
 
Kamanda wa polisi Mkoa wa Mbeya Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Ahmed Msangi ametoa wito kwa jamii kufunika pamoja na kufukia mashimo yaliyo wazi kwa kuwa ni hatari kwa watoto na hata watu wazima.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post