KILELE CHA MAADHIMSHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI KUFANYIKA KIZUMBI KATIKA WILAYA YA SHINYANGA

 
Zikiwa zimesaria siku chache ili kufikia kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani siku ya Jumamosi wiki hii tarehe 8,mwezi huu,wakazi wa Shinyanga wameombwa kujitokeza kwa wingi katika maadhimisho hayo ambayo katika wilaya ya Shinyanga yatafanyika katika uwanja wa michezo shule ya msingi Nhelegani kata ya Kizumbi kuanzia saa tatu asubuhi.

Akizungumza leo katika kikao cha maandalizi ya sherehe hizo kilichofayika katika ukumbi wa ofisi ya afisa matendaji kata ya Ngokolo mjini Shinyanga,mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya sherehe hizo katika wilaya ya Shinyanga bwana Mtinga Masatu ambaye ni mwenyekiti wa mtandao wa asasi za kiraia katika manispaa ya Shinyanga-SHIMUNGONET  amesema ni vyema wananchi wote wanawake kwa wanaume wakahudhuria maadhimisho hayo.

Masatu amesema mgeni rasmi katika maadhimisho hayo anatarajiwa kuwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga Bi Anna rose Nyamubi na kuongeza kuwa siku hiyo kutafanyika maandamano kuanzia ofisi ya mtendaji kata ya Kizumbi kuelekea kwenye uwanja wa Michezo wa shule ya msingi Nhelegani.

Masatu ameongeza kuwa katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani katika manispaa ya Shinyanga,mbali na kufanyika kwa maandamano hayo pia kutakuwepo na shughuli mbalimbali kama vile maonesho ya bidhaa za wanawake wajasiriamali,upimaji hiari wa VVU,burudani na mambo kadha wa kadha ambayo wamejipanga vyema katika kuhakikisha siku hiyo inafana kweli kweli.
 Ametumia fursa hiyo kuwaomba wakazi wote wa Shinyanga kujitokeza kwa wingi siku hiyo na kuongeza kuwa wale watakaopata nafasi basi wawahi eneo la benki ya NBC mjini Shinyanga kusubiri usafiri wa kuwapeleka eneo la tukio kuanzia saa moja na nusu asubuhi hadi saa mbili asubuhi

Aidha mwenyekiti huyo SHIMUNGONET amesema  ujumbe wa siku ya wanawake mwaka huu ni "Chochea mabadiliko kuleta usawa wa kijinsia".

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post