Kikundi cha
Makhirikhiri kutoka kijiji cha
Bulimba kata ya Ukenyenge wilayani Kishapu ambacho kwa sasa ni maarufu
sana kwa burudani kikimpokea mkuu wa mkoa katika eneo la mkutano wa hadhara
katika kijiji cha Bubinza wilayani Kishapu.
|
Mwenye suti ni mkuu wa wilaya ya Kishapu Wilson Nkhambaku baada ya mzuka kupanda akavunja ukimya na kuamua kucheza ngoma ya Makhirikhiri kutoka kijiji cha Bulimba kata ya Ukenyenge wilayani Kishapu
Mkuu wa wilaya ya Kishapu Wilson Nkhambaku akimkaribisha
mkuu wa mkoa wa Shinyanga ili azungumze na wananchi wa kijiji cha Bubinza
ambako leo kumefanyika uzinduzi wa wiki ya maji duniani.Pamoja na mambo mengine
mkuu huyo wa wilaya aliushukuru uongozi wa mkoa wa Shinyanga kwa kuchagua
wilaya ya Kishapu kati ya halmashauri 6 za mkoa
kuwa mwenyeji wa siku ya uzinduzi wa wiki ya maji kimkoa.
|
Mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Nassoro Rufunga kabla ya hotuba yake akikabidhi pesa jumla ya
shilingi elfu 80 kwa kikundi cha Burudani cha MakhiriKhiri.a(kiongozi wao anapokea)Hii ni baada ya kufurahishwa na kazi yao,wageni
mbalimbali walioambatana na mkuu wa mkoa wakakusanya kile walichokuwa nacho
kwenye mifuko yao kwa ajili ya kuwapongeza vijana hao ambao kiukweli wanajua
wanachokifanya mithili ya makhirikhiri wa nchini Botswana.
Wananchi wakifuatilia kilichokuwa kinajiri katika uzinduzi huo
Aliyesimama ni mkuu wa mkoa wa Shinyanga Ally Nassoro Rufunga akizungumza na wananchi wa kijiji ch Bubinza ambapo pamoja na mambo mengine aliwataka watunze mradi huo huku akisisitiza wananchi katika halmashauri zote za wilaya katika mkoa wa Shinyanga kupanda miti katika maeneo yanayozunguka miradi ya maji ili kutunza uoto wa asili
Mkuu wa mkoa (mwenye suti nyeusi upande wa kulia)akitoa hotuba yake katika kijiji cha Bubinza wilayani Kishapu |
Baada ya hotuba ya mkuu wa mkoa wa Shinyanga Makhirikhiri wakaendelea kufanya yao |
Wananchi wakifuatilia kilichokuwa kinajiri katika eneo la tukio |
Wageni mbalimbali wakiwemo wakuu wa idara za ulinzi na usalama mkoani Shinyanga wakiangalia kikundi cha Makhirikhiri.
Katika kuadhimisha wiki ya maji kesho tarehe 16 kutakuwa na
uzinduzi wa mradi wa maji wa Mwamalili/Seseko katika manispaa ya Shinyanga,Machi
18 katika kijiji cha Bulekela wilayani Kishapu,Machi 19 kijiji cha Mwamashele
manispaa ya Shinyanga,Machi kijiji cha Mishepo wilaya ya Shinyanga,Machi 21
kijiji cha Ibadakuli,Nhelegani katika manispaa ya Shinyanga na Machi siku ya
kilele cha wiki ya maji ni katika kijiji cha Kagongwa/Iponya ambapo mbali na
kuzindua miradi katika vijiji hivyo pia kutafanyika mikutano ya hadhara
sambamba na kuhamasisha wananchi(elimu kuhusu umuhimu wa kuchangia fedha kwa
ajili ya mfuko wa maji)
|