Msako!!! WAHALIFU KIBAO WAKAMATWA GEITA,WENGI WAO NI VIJANA,JESHI LA POLISI MKOA HUO LAWAOMBA WANANCHI KUENDELEA KUTOA USHIRIKIANO

Kamanda wa polisi mkoa wa Geita-Leonard Paul
Jeshi la polisi mkoani Geita limewaomba wananchi kuendelea kutoa ushirikiano kwa jeshi hilo katika misako inayoendelea kufanywa na jeshi la polisi ambapo kati ya tarehe 22 hadi 28 mwezi januari wamefanikiwa kukamata wahalifu 10.

Wito huo umetolewa na kamanda wa polisi mkoa wa Geita Leonard Paul wakati akitoa  taarifa kwa waandishi wa habari kuhusu kukamatwa kwa wahalifu mkoani Geita ambapo wananchi kwa kushirikiana na jeshi hilo wamefanikiwa kuwatia mbaroni watu kumi katika kipindi hicho cha Januari 22 hadi 28 mwaka huu.

Kamanda Paul amewataja watuhumiwa wa uhalifu wa aina mbalimbali waliokamatwa kuwa  ni Goodluck Faustine(18) Venance Daniel(18) Fabiani Raphaeli(18) Hamis Idd(18) George Manase(19) Abeid Prosper(19)Kashindye Juma(20) Faida Charles(20) Mhoja Kadogo(19) na Baasi Ally(18).

Kamanda amevitaja vitu ambavyo watuhumiwa hao wamekamatwa navyo kuwa ni pamoja na Tv  flat screen 4, tv za kawaida 3 ,deck za dvd 4 sub-woofer 2 simu za mkononi 2, mashine ya kunyolea 1 ,vifaa vya kuvunjia nyumba ambavyo ni sululu 1,nondo1 mkasi mkubwa 1, spana5 plaiz 1 na tayari baadhi ya wananchi wameanza kuvitambua vitu vyao vilivyoibiwa.

Katika hatua nyingine baadhi ya wananchi katika mkoa wa Geita wamesema wamekuwa wakishangazwa kuona watuhumiwa wengi kuwa na umri unaofanana na hiyo yote inatokana na lindi la vijana ambao hawana kazi kujiingiza katika uharifu ili waweze kujipatia vipato vya kujikimu.

Kwa upande wake ambaye ni katibu wa shirika lisilo la kiserikali la kutetea haki za binadamu wilayani Geita Bwana Elineema Charles amesema kutokana na mji wa Geita sasa hivi unavyokuwa kwa kasi ni vyema  jeshi la polisi likashirikiana na raia ili kufichua vitendo vya uharifu ambavyo vinaweza kuhatarisha sio mali tu za wananchi lakini hata maisha.

Hata hivyo bw charles ameongeza kuwa ushiriki wa kamanda wa polisi mkoani Geita ni vyema ukaigwa na askari wote wa mkoa huu hata nchi kwa ujumla kwani kila mara amekuwa mwepesi wa kufika kwenye matukio mbalimbali yanayojiri katika mkoa huo kwa kujionea mwenyewe na si kuambiwa kama walivyo wengine.

Na Valence Robert-Geita

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post