Ajali tena Singida!! BASI LA ZUBERI LAPINDUKA LIKIMKWEPA BIBI KIZEE

NB picha haiendani na tukio la ajali ya leo
Bus kampuni ya Zubery lenye namba za usajili T 119 AZZ lililokuwa likitokea jijini Mwanza kwenda jijini Dar es salaa , limepinduka leo majira ya saa 7 mchana wa leo eneo la Isuna wilaya ya Ikungi mkoani SINGIDA na mpaka sasa taarifa tulizonazo ni kwamba takribani watu 2 kati ya 60 waliokuwemo ndani ya basi hilo wameripotiwa kufariki dunia papo hapo eneo la tukio.

Habari kutoka eneo la tukio zinasema kuwa  chanzo cha ajali hiyo ni baada ya basi hilo kutaka kumkwepa bibi kizee aliyekuwa anakatiza barabara ndipo lilipopinduka.

Walioshuhudia tukio hilo wamesema ajali hiyo imehusishwa na imani za kishirikina kutokana na kile kilichodaiwa kuwa baada ya ajali hiyo bibi huyo alirudi nyuma mara ya pili na kusababisha ajali hiyo kisha kukaa kwa muda mrefu katika eneo la tukio.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post