Mauaji ya kutisha Kahama !!! WANANCHI WAUA WATU WAWILI KWA TUHUMA YA WIZI,TUNAOMBA RADHI KWA PICHA ZINATISHA

Miili ya marehemu hao baada ya kupakizwa katika gari la polisi wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga
Gari la polisi wilaya ya Kahama likiwa limezungukwa na wananchi eneo la tukio
Watu wawili wanaosadikiwa kuwa ni wezi wameuawa kwa kushambuliwa na wananchi waliojichukulia sheria mkononi kwa kisingizio cha kuwa na hasira kali katika mtaa wa Mayila kata ya Nyihogo wilayani Kahama Mkoani Shinyanga.

Tukio hilo la mauaji limetokea leo majira ya saa tisa alasiri baada ya vijana hao kuhisiwa kuhusika na matukio ya wizi ambayo yamekuwa yakitokea katika eneo hilo mara kwa mara na kuwakosesha amani wananchi.

Kwa mujibu wa Diwani wa Kata ya Nyihogo Amos Sipemba, aliyefika eneo la tukio mara baada ya mauwaji hayo, amesema hadi sasa mmoja wa marehemu ametambulika kwa jina la Joseph Bakuku huku mwingine akiwa bado hajafahamika.

Sipemba amesema huenda kufanyika kwa mauaji hayo kunatokana na wananchi hao kuwahisi vijana hao kuhusika katika matukio mawili ya uvamizi yaliyotokea usiku wa kuamkia jana katika kata hiyo na kuripotiwa ofisini kwake.

Jeshi la Polisi wilayani Kahama limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba miili ya marehemu hao imehifadhiwa katia chumba cha kuhifadhia maiti cha hospitali ya Wilaya ya Kahama, huku uchunguzi wa tukio hilo ukiendelea.
Credit-Dunia kiganjani 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post