Historia kuwekwa Shinyanga!!! KIWANDA CHA NYAMA CHA TRIPLE 'S' CHA MWAKA 1975 KUANZA KUFANYA KAZI MWEZI UJAO


Katika kile kinachoweza kusimuliwa na wakazi wa mkoa wa Shinyanga kama historia ama wengine kudhani pengine ni kama ndoto,hatimaye kiwanda cha  nyama  cha Triple  ‘S’ kilichopo ndani ya manispaa ya Shinyanga ambacho  kilichojengwa mwaka 1975 na hakijawahi kufanya kazi hata siku moja kinatarajiwa kufunguliwa na kuanza kufanya kazi mwezi machi mwaka huu.

Akizungumza  jana mbele ya waziri wa maendeleo ya mifugo na uvuvi  Titus Kamani  wakati wa ziara yake mkoani Shinyanga  alipotembelea kiwanda hicho mmiliki wa  kiwanda hicho Salum Seif  amesema anatarajia kufungua na kuanza kazi  mwezi Machi mwaka huu na kuongeza kuwa  kiwanda hicho kina uwezo kwa kuchinja ng’ombe 250 hadi 300 kwa siku ila kwa kuanza wataanza na  ng’ombe 50 kila siku.

Waziri wa maendeleo ya mifugo na uvuvi  Titus Kamani alitumia fursa hiyo
kuwataka wafugaji watumie kiwanda cha nyumbani  kinachoweza kuchukua mifugo yao pamoja na kuwepo kwa changamoto ya  ng’ombe wa hapa nchini kukosa ubora  wa kuingia kwenye ushindani wa soko la nyama hivyo kuwataka wafugaji kubadilisha mfumo wa ufugaji na kuwa wa kibiashara  ili waweze kunyanyua uchumi wa mkoa wa Shinyanga  na mtu mmoja mmoja.


Naye  mkuu wa wilaya ya Shinyanga Anna Rose Nyamubi alimtaka mwekezaji huyo kuwaelimisha wananchi  walio kando kando ya kiwanda hicho kwa kupitia afisa maendeleo  ya jamii kwa kutenga  maeneo ya kuendeleza shughuli zao ili kuweza kuepusha migogoro isiyokuwa ya lazima pia wafugaji nao  kuelimishwa ili waweze kunufaika na kiwanda hicho.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post