Diwani wa kata Chigunga Hoja Mlyakalamu
kupitia tiketi ya CCM anatuhumiwa kuiba mabati 14 kutoka katika mfuko wa jimbo
uliotolewa na mbunge wa jimbo hilo mh, Lolecia Bukwimba katika jimbo la Busanda
wilayani Geita na
ameamriwa ayarudishe ndani ya siku 14
baada ya kukiri jambo ambalo hadi sasa hajalitekeleza.
Tuhuma hizo zimefahamika mara baada ya
mbunge huyo kutembelea shughuli za maendeleo katika jimbo lake na alipofika
katika kijiji cha kayenze alipokuwa amesubiriwa kwa hamu tangu ubadhirifu huo
utokee walimuueleza kwenye mkutano wa hadhara kuwa mabati uliyotoa katika shule
ya msingi Sanza ni mangapi?
Taarifa kutoka kwa afisa mtendaji wa kata
hiyo Bw William Mabilika alisema kuwa wao katika kikao cha maendeleo ya kata
WDC walikaa na kuidhinisha kuwa mabati yakanunuliwe 100 ya geji 28 na muhtasari
unasomeka hivyo na baada ya hapo wakamtuma diwani akiwa kama mwakilishi wa
wananchi ili ayafuate mjini Geita waliponunulia.
Afisa mtendaji huyo alisema walishangaa
kuona mabati 86 ya geji 30 tofauti na walivyokuwa wamekubaliana na inadaiwa kuwa
waliyanunua kwenye duka la Kwilasa ambaye ni mwenyekiti wa halmashauri ya mji
wa Geita.
Kwa upande wa mratibu elimu kata ya
Chigunga Bw John Rugila amesema kuwa ni kweli walipewa sh milioni 2 na laki
tano kwa ajili ya kununua mabati 100 katika shule ya msingi
Sanza ili waezeke yenye geji 28 lakini ameshangaa kuona mabati 86 na geji 30.
‘’Ndugu
mwandishi hata na mimi nashangaa kuona mabati pungufu tofauti na ilivyokubaliwa
katika vikao vyetu vya WDC’’,alisema mratibu huyo wa kata.
Diwani huyo alipoulizwa kuhusiana na
tuhuma hizo alikiri kwenda kinyume na makubaliano ya kikao yeye akaleta mabati 86 badala ya 100 na
yenye geji 30 badala ya 28 kama alivyoagizwa na WDC na kujitetea kuwa pesa
zingine alitumia kwenye usafiri wa kuyasafirisha kutoka Geita hadi Kayenze.
Aidha diwani huyo alipolizwa na waandishi wa
habari kwamba je hizo geji 30 badala ya
28 zimehusikaje katika gharama za usafiri,diwani huyo hakuwa na jibu.....akasema
“ Hata hivyo nimeamuriwa kuyarudisha
mabati 14 tatizo lako ni nini? Alisema diwani huyo.
Hata hivyo alivyoulizwa tena kwa vile
anarudisha mabati 14 tu na geji 30 atayarudisha achukue geji 28? Alisema
hana hela ziliisha.
Mbunge wa jimbo hilo Lolesia Bukwimba
alisema amepokea malalamiko kutoka kwa wananchi kwenye mkutano wa hadhara kwamba
kuna upungufu wa mabati hayo na tofauti ya geji walizokubaliana na kwamba diwani huyo alikiuka na hadi sasa
shule hiyo haijajengwa.
“Diwani
huyo aliwahi kufanya mkutano hapo na kuwaambia ameleta mabati 86 kutoka kwa
mbunge na 14 yaliyobaki atakuja nayo mbunge na ndipo nilipofika bila mabati
wananchi wakaniuliza mabati yako wapi tuliyoambiwa na diwani utakuja nayo?”,aliongeza
mbunge huyo
Kufuatia maswali hayo ya wananchi, mbunge
alilazimika kutoa majibu kwamba yeye tayari alishatoa mabati 100 na yote yalishakuja
wananchi wakamwambia kuwa aende na diwani wake na baada ya hapo mbunge huyo
alimsimamisha diwani na kumuuliza kuhusu mabati hayo.
‘’Ndugu
mwandishi niliagiza baada ya kupata malalamiko kutoka kwa wanachi kwenye
mkutano wa hadhara diwani alete hayo mabati ndani ya siku 14 kwani aliwadanganya
hao wananchi na kunisingizia mimi kuwa nitakuja nayo mabati lakini hadi sasa
hivi sijapata taarifa za kurudisha kwa mabati hayo’’ ,alisema mbunge huyo.
Na Valence Robert-Geita
Na Valence Robert-Geita
Post a Comment