VIJANA WA CCM SHINYANGA MJINI WATOA MSAADA KWA WATOTO WENYE ULEMAVU WA NGOZI KATIKA KITUO CHA BUHANGIJA




Kwa mara kwanza umoja  wa vijana wa CCM  ( UVCCM) wilaya ya Shinyanga mjini  umeadhimisha sherehe za kutimiza miaka 37 ya Chama cha mapinduzi CCM katika kituo cha watoto wenye ulemavu wa ngozi  cha Buhangija jumuishi kilichopo mjini hapa  kwa kufanya usafi pamoja  katika kituo hicho samabamba na kutoa msaada wa vyakula.

Umoja huo umetoa kilo hamsini za mchele pamoja na mafuta ya kupikia lita kumi vyote vikiwa na thamani ya shilingi elfu themanini na saba pamoja na kupanda miti 30 ya matunda na kivuli katika kituo hicho hapo jana

Mwenyekiti wa umoja huo bwana  Abubakari Mkadam amesema wameona vyema kuadhimisha sherehe hizo za miaka 37 ya CCM kwa kutembelea katika kituo hicho cha walemavu wa ngozi kwa kufanya usafi wa mazingira, kupanda miti kufua nguo pamoja na kugawa chakula ,kwa lengo la kushiriki nao sherehe hizo za kuzaliwa kwa CCM na kwamba sherehe nyingi za CCM zimekuwa zikiadhimishwa kwa kufanya mikutano mbalimbali ya wananchi lakini  kwa mwaka huu (2014)  wao wameona wafanye tofauti kwa kuwatembelea vijana wenzao ambao huishi katika mazingira magumu na hatarishi.

Hata hivyo mkuu wa kituo hicho  cha walemavu Briton Mduma amezitaja changamoto kubwa zinazowakabili vijana hao walemavu kuwa ni uhaba wa chakula, vifaa vya kufanyia usafi ,vyandarua, pamoja na upungufu wa vitanda ambapo kuna watoto 258 huku kukiwa na vitanda 60 na kuwa lazimu kulala  wane wane hadi watano katika kitanda kimoja.

Naye mmoja wa watoto hao wenye ulemavu ngozi katika kituo hicho Semen Deus amewashukuru vijana hao wa UVCCM kuwatembela katika kituo hicho na kukishukuru chama tawala kwa kuwakumbuka katika siku za maadhimisho yake huku akitoa wito kwa vyama vingine kuiga mfano huo .

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments