MZEE AJINYONGA KWA CHANDARUA HUKO MASKATI

NB Siyo mti aliojinyonga marehemu
Mkazi  mmoja wa kijiji  cha Maskati maarufu kwa jina la Maskati Fisi  kata ya Imesela katika wilaya ya Shinyanga  vijijini Njile Nkelembi(55-60 amekutwa  amefariki dunia kwa  kujinyonga kwa kutumia chandarua katika mti wa mwembe .

Tukio hilo limetokea jana majira ya saa moja ambapo Njile Nkelembi ambaye alikuwa anafanya kazi ya kuuza kahawa  katika kijiji hicho alikutwa amejinyonga katika  shamba lake jirani na nyumba yake.

Akizungumza na malunde1.blogspot.com mwenyekiti wa  kijiji hicho Hamis Salum amesema hadi sasa hakuna sababu iliyopelekea kutokea kwa kifo hicho.

Naye Diwani wa kata ya Imesela Juma Kayumbo  ameeleza kusikitishwa na taarifa ya kifo hicho na kuongeza kuwa chanzo cha kifo hicho bado hakijajulikana waziwazi kwani marehemu hakuacha ujumbe wowote na kwamba tayari mazishi yamefanyika.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post