Mke wa mtu sumu!! JAMAA AUAWA KWA KUKATWA PANGA USONI BAADA YA KUBAMBWA NA MKE WA MTU


Mwanamme mmoja aliyejulikana kwa jina la James Juma (25-30) mvuvi ameuawa kwa kukatwa panga sehemu za usoni na mkono wa kulia mara baada ya kubainika ana mahusiano ya kimapenzi na mke wa mtu katika kijiji cha Nkome mkoani Geita.

Kamanda  wa polisi mkoa wa Geita Leonard Paul amesema tukio hilo limetokea juzi majira ya  saa moja na nusu usiku  katika kitongoji cha Jakalanda  kijiji cha Nkome wilayani Geita ambapo James Juma  mkazi wa kijiji jirani cha Ihumilo aliuawa kwa kukatwa panga na Makaranga Charles(30-35).

Amesema tukio hilo limetokea baada ya Makaranga  kumhisi James Makaranga kuwa anatembea na mkewe Regina Revocatus kwa muda mrefu ndipo mtuhumiwa aliamua kuweka mtego na kumkuta marehemu  katika mazingira yaliyomfanya kutekeleza mauaji hayo.

Mwenyekiti wa kitongoji hicho  Lucas Mbodi ameeleza kuwa hadi sasa mwili wa marehemu wameuchukua na kumpeleka kwake kijiji cha Ihumilo ambapo mazishi yatafanyikia huko kwa mkewe.

Hadi  hivi sasa mtuhumiwa na mkewe wametoroka na hawajulikani walipo na jeshi la polisi linaendelea kuwatafuta watuhumiwa hao.


Na Valence Robert-Geita

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post