MCHEZO WA LIGI DARAJA LA KWANZA KATI YA STAND UNITED YA SHINYANGA NA KANEMBWA JKT YA KIGOMA WAPIGWA KALENDA




Shirikisho la mpira wa miguu Tanzania (TFF) limesogeza mbele mchezo wa marudiano wa daraja la kwanza kati ya Stand United na Kanembwa JKT ulipangwa kuchezwa tarehe 1 mwezi Februari mwaka huu katika uwanja wa Ally Hassan Mwinyi mjini Tabora.

Kwa mujibu wa taarifa ya Shirikisho hilo iliyotolewa tarehe 28 mwezi huu, na katibu mkuu wa wa shirikisho hilo Mwesigwa Selestine kwa timu hizo mbili  mchezo huo wa marudiano  utapangiwa tarehe nyingine huku akizitaka timu husika na wasimamizi wa mchezo huo wasiende katika kituo cha Tabora.
Na Isaac wa Edo,Shinyanga

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post