MAZISHI YA MWIGIZAJI WA FUTUHI MZEE DUDE ALIYEFARIKI JUZI YAFANYIKA JIJINI MWANZA



Dua ya kuuombea kheri mwili wa aliyekuwa mwigizaji wa kundi la uchekeshaji wa luninga la FUTUHI marehemu Omary Majuto al maarufu kwa jina la Mzee Dude ilifanyika  majira ya saa 9:00 nyumbani kwake Ilemela jijini Mwanza ikiwa kabla ya mazishi yaliyofanyika jana jioni majira ya saa 10:00.
Awali kabla sala maalum ilifanyika.
Waigizaji mbalimbali wa sanaa mbalimbali wameshiriki akiwepo Mc. Katumba ambaye anaonekana akiwa na wasanii wa kundi la BABATAN Itagata, Kafuku Kahualanga na Mwanshum ambao walifanya kazi na marehemu kwenye kundi la FUTUHI (kabla hawajajiengua) na wa kwanza kulia ni Tatu wa FUTUHI.
Ni wakati wa kuusitiri mwili wa aliyekuwa mwigizaji wa kundi la uchekeshaji wa kundi la FUTUHI marehemu Omary Majuto al maarufu kwa jina la Mzee Dude, katika makaburi ya Iloganzala wilayani Ilemela jijini Mwanza.



Kwa mapenzi mema na urafiki hata watoto wadogo walishiriki kuweka mchanga kuusitiri mwili wa aliyekuwa mwigizaji wa kundi la uchekeshaji wa  FUTUHI marehemu Omary Majuto al maarufu kwa jina la Mzee Dude aliyefariki juzi jioni majira ya saa 11 jioni

Katika mazishi hayo Beat Agenda iliwakilishwa naye DVJ Bavon (mwenye skafu na kofia kushoto).
Shekhe wa wilaya ya Ilemela Shk. Mohamed Yusufu akitoa neno la barka kwa waliohudhuria mazishi hayo
Baadhi ya watoto wa marehemu wakijumuika na wajukuu na marafiki wengine wa marehemu katika sala ya kuhitimisha maziko kifamilia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post