Ukatili wa Kutisha!! BABA WA KAMBO AUA MTOTO KISA ANAMPIGIA KELELE WAKATI WA KULALA


NB-Picha haiendani na habari hapa chini
Mtoto mmoja mwenye umri wa miaka miwili  mkazi wa Kijiji cha Majalila wilaya ya Mpanda mkoani Katavi ameuawa kwa kupigwa na fimbo kwenye sehemu mbalimbali za mwili wake  na baba yake  wa kambo  aitwaye  Hamisi Mohamed.

Tukio hilo lilitokea hapo juzi majira  ya usiku wakati moto huyo  alipokuwa amelala kitandani na wazazi wake.
 
Kwa mujibu wa kamanda wa polisi wa mkoa wa katavi Dhahiri Kidavashari alisema marehemu huyo alikufa baada ya baba yake wa kambo kukasirishwa na kitendo cha mtoto huyo kulia wakati akiwa amelala kitendo ambacho aliona kinamnyima usingizi.

Alisema kitendo hicho cha  mtoto kulia kilimfanya baba huyo wa kambo kimkasirishe na ndipo alipoanza kumpiga fimbo sehemu mbalimbali za mwili wake huku mama wa motto akimsihi baba huyo wa kambo aache kumpiga mtoto huyo.

Alieleza baada ya kuona hali ya motto  huyo imekuwa mbaya baba huyo wa kambo alimuaga mkewe kuwa anakwenda dukani kumnunulia dawa  za maumivu.

Baada ya baba huyo wa kambo kwenda dukani mtoto huyo alifariki ikiwa ni  muda mfupi tu toka baba yake huyo wa kambo alivyokuwa amekwenda dukani ambapo alitokomea kusiko julikana.

Kamanda Kidavashari alisema uchunguzi wa awali  wa baba wa kambo  kumuua mtoto huyo ni chuki baina ya mama wa mtoto huyo aitwaye Diana Philipo  na mume wake  ambaye hakutaka marehemu aishi nyumbani kwake.

Jeshi la polisi linaendelea kumtafuta mtuhumiwa ili likimkamata limfikishe kwenye vyombo vya sheria .

Na   Walter Mguluchuma.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post