MAZISHI YA BIBI MWENYE MIAKA 104 ALIYEKUWA ANALELEWA NA ASKOFU MWOMBEKI YAFANYIKA KIJIJINI KWAKE

Askofu Edson Mwombeki  wa kanisa la Emanuel lililopo mjini Shinyanga akiwa nyumbani  Bi Martha Kapuya enzi za uhai wake baada ya Askofu huyo kumshauri bibi huyo aache maisha ya kuombaomba mjini,akaanza kumpatia malazi na chakula kizuri


 BI Martha Kapuya (104) mkazi wa  kijiji cha Uzogore Bujiga  Enzi za uhai wake baada ya kuanza kulelewa na Askofu MWOMBEKI akiwa ni miongoni mwa vikongwe 108 anaowalea  katika  manispaa ya Shinyanga waliojitenga na jamii kwa hofu ya  kuuawa kutokana na imani za kishirikina

Mwili wa marehemu Martha Kapuya  aliyefariki mwishoni mwa wiki iliyopita akiwa na umri wa miaka 104  ukiwa kwenye jeneza kabla ya mazishi hapo jana nyumbani kwake katika  kijiji cha Uzogore Bujiga ndani ya manispaa ya shinyanga
 Watu wenye mapenzi mema waliohudhuria mazishi ya bi Martha aliyekuwa akilelewa na Askofu Mwombeki wa Kanisa la Emmanuel,ambapo kabla ya hapo alikuwa anaishi mjini shinyanga kwa kuombaomba na alikimbia makazi yake kwa hofu ya kuuawa kutokana na imani za kishirikina kwani alikuwa na macho mekundu.
 Askofu Mwombeki akiongoza ibada ya mazishi katika kijiji cha Uzogore Bujiga ambapo aliiomba jamii kuwajali wazee ili waweze kuishi maisha marefu kama ilivyokuwa kwa bibi Martha ambaye amefariki akiwa na umri wa miaka 104 kutokana na umri wake kuwa mkubwa lakini kabla ya hapo alikuwa ametengwa na jamii lakini askofu huyo akachuchua jukumu la kumlea akiwa ni miongoni mwa vikongwe 108 anaowalea katika manispaa ya shinyanga.
 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments