BREAKING NEWS.....GEITA KIMENUKA.........

Mapigano makali yameibuka kati ya waislamu na wakristu kuhusu uchinjaji,katika eneo Buseresere- GEITA.

Kuna mapigano makali yanaendelea muda huu kati ya waislamu na wakristu kuhusu kuchinja.
Misikiti mingi imebomolewa na inasemekana watu kadhaa wameshauawa.
 
Taarifa ambazo zimetufikia hivi punde zinaeleza kuwa huko mkoani Geita, kuna vita kati ya Waislamu na Wakristo, kufuatia hatua ya Wakristo kuchinja mifugo kwa nia ya kuuziana wenyewe kwa wenyewe kwenye bucha walilotenga.

Jambo hilo linaelezwa kuzua tafrani kwa jamii ya Waislamu, kwani waliamua kuvamia eneo hilo na kuharibu bucha, pikipiki eneo hilo, na kusababisha watu kuingilia, na vita kuibuka, silaha za jadi zikitumika.
KWANINI ?
Wakristo Mkoani Geita eneo la Katoro na Buselesele, waliamua kuachana na kununua nyama katika bucha za kawaida kwa madaikwamba hiyo ni ibada kwa waislamu, na hivyo wao hawako tayari kushiriki ibada hiyo, na badala yake watafanya ya kwao. Ndipo walipokwenda Kituo cha Polisi na kuomba kibali cha kuchinja, ambacho walipewa ilmradi wasiuze nyama hiyo.

hatimaye Wakrsito hao wakachinja na kuamua kupeleka kwenye bucha lao ambalo wamelitenga kwa ajili ya waumini wao kununua. Waislamu kuona hivyo, ndipo wakaenda kuripoti kituoi cha Polisi, na wakati Polisi (wachache) wanaongea na viongozi wa Kikristo eneo hilo ili kutatua na kurejesha amani, ndipo kundi la Waislamu likaja na kuanza kushambulia kilichokkuwa eneo hilo, wakivunja bucha, na pikipiki ya mkristo mmojawapo iliyokuwa eneo hilo.

Hatua hiyo imeelezwa kuibua hasia na kupelekea baadhi ya wat waliokuwa eneo hilo kuanza kujibu mashambulizi hayo, na mpaka hivi sasa inaripotiwa kuwa nguvu zaidi ya Jehi la Polisi haijafika eneo hilo, huku waumini wawili wa dini ya Kiislamu wakiwa katika hali mbaya kutokana na kipigo.

Silaha ni za jadi, na eneo hilo haliko salama kwa hivi sasa, kwani hata amduka mengine yamefungwa kuhofia usalama wa mali na maisha.

Katibu wa umoja wa makanisa ya Katoro na Buselesele, Mchungaji Silvanus Dominick, ameeleza kuwa kama hali haitatulizwa mara moja basi eneo hilo laweza kuleta madhara zaidi.
 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments