AJINYONGA KWA KUTUMIA KIPANDE CHA CHANDARUA-SHINYANGA

Mwanamme mmoja aitwaye Moshi Andrew (28) mkazi wa kijiji cha Mpera kata ya Isagehe wilayani Kahama mkoani Shinyanga amekutwa akiwa amekufa kwa kujinyonga kwa kutumia kipande cha chandarua.

Walioshuhudia tukio hilo wamesema mnamo Januari 16 mwaka huu majira ya saa 12 asubuhi walikmkuta mtu huyo akiwa amejinyonga juu ya dari ndani ya nyumba yake kwa kutumia kipande hicho cha chandarua.

Jeshi la polisi mkoani Shinyanga limethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kwamba chanzo cha tukio bado kinachunguzwa na hakuna mtu anayeshikiliwa kuhusiana na tukio hilo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments