Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

NDOA 130 ZAFUNGWA,KATAMBI ASISITIZA MAADILI


Jumla ya Ndoa 130 zimefungwa leo jijini Dar es Salaam wakati wa Ibada ya Ndoa iliyoandaliwa na Taasisi ya Al-Hikma inayoongozwa na Rais Taasisi hiyo, Sheikh Shareef Abdulgadir, ambapo Mgeni Rasmi ni Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Patrobass Katambi.

Akizungumza baada ya ibada hiyo,Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi,Patrobass Katambi alisisitiza msingi wa maadili uanzia katika familia ambapo ameipongeza taasisi ya Al-Hikma kwa kuwezesha zoezi hilo wakianzia na utaratibu wa awali ambao ulihusisha mahojiano na uchunguzi wa kina,kuwalipia mahari Vijana hao wa kiume na mahojiano maalumu ikiwemo wanandoa hao na wenza wao.

“Nitumie fursa hii kutoa pongezi zangu za dhati kwenu Taasisi ya Alhikma katika zama za sasa,changamoto ya mmomonyoko wa maadili kwa asilimia kubwa inachochewa na ongezeko la mahusiano yasiyo halali, migogoro ya kifamilia na mambo mahususi yanayowakabili viana,ndoa kama hizi ni sehemu ya suluhisho.”amesema Waziri Katambi

“Ndoa halali ni sababu ya mahusiano na kizazi halali kinachojenga familia halali ambayo ndiyo msingi wa kwanza wa jamii imara. Familia ikisimama vizuri jamii itasimama vizuri, na ikiwa hivo, taifa nalo litastawi na kuimarika” aliongeza Waziri Katambi

Ndoa hizo 130 zimefungwa jijini Dar es Salaam katika wilaya ya Temeke huku viongozi mbalimbali wa serikali,dini na wananchi wamehudhuria hafla hiyo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com