Na mwandishi wetu,Dodoma
Katika kipindi cha Julai 2025 hadi Aprili 2026, Jumla ya Jumuiya za Kiraia 126 zimesajiliwa Nchini, 12 kati yake zikiwa ni Jumuiya za kidini na 114 zisizo sa kidini.
Takwimu hizo zimebainishwa leo Jumatatu Mei 25, 2026 Bungeni Mjini Dodoma na Waziri wa mambo ya ndani ya Nchi Mhe. Patrobas Katambi wakati akisoma hotuba ya bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka 2026/27, akibainisha kwamba ukaguzi wa jumuiya 350 ulifanyika na Wizara yake katika kipindi kama hicho cha Julai 2025 hadi Aprili, 2026, lengo likiwa ni kufuatilia utekelezaji wa masharti ya usajili pamoja na kubaini mchango wa Jumuiya hizo katika maendeleo.
"Mhe. Spika, pia Wizara imeanzisha programu za ushirikishwaji ili kuimarisha uelewa na uwajibikaji wa viongozi wa jumuiya za kiraia katika uendeshaji wa jumuiya zao. Kupitia programu hiyo, jumla ya viongozi wa jumuiya za kidini na zisizo za kidini 2,500 walipatiwa mafunzo kuhusu uendeshaji wa jumuiya unaozingatia sheria na kuimarisha amani, utulivu na mshikamano wa kitaifa.
Katika mwaka 2026/27, Wizara imetenga Shilingi bilioni 1.57 kwa ajili ya shughuli za usimamizi na uratibu wa Jumuiya za Kiraia nchini." Amesema Waziri Katambi.

Social Plugin