Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

FOUNTAIN GATE FC YAJIANDAA KWA VITA YA MECHI ZA MWISHO LIGI KUU

Na Bora Mustafa, Arusha.

Kocha Mkuu wa Fountain Gate FC, Felix Minziro amesema licha ya timu yake kukabiliwa na changamoto ya kikosi kuwa kipana, muda wa mapumziko walioupata umeisaidia timu kujiandaa vyema kuelekea michezo iliyosalia ya Ligi Kuu. 

Amesema miongoni mwa michezo hiyo ipo dhidi ya vigogo kama Azam FC pamoja na Young Africans SC katika mechi tano za mwisho wa msimu.

Akizungumza Minziro amesema hayo Leo 25, mei, ,2025  jijini Arusha ambapo timu hiyo imeweka kambi maalum kwa ajili ya kuimarisha utimamu wa mwili na akili kwa wachezaji wake baada ya ratiba ngumu ya michezo ya mfululizo..

 Pia amesema mapumziko ya wiki moja yaliyopatikana yamekuwa msaada mkubwa kwa wachezaji kurejea kwenye kiwango kizuri kabla ya kuendelea na mechi zilizobaki.

Hata hivyo, Minziro amebainisha kuwa changamoto kubwa waliokuwa nayo si majeraha makubwa bali ni uchovu pamoja na majeraha madogomadogo yaliyotokana na ushindani wa ligi hiyo.

 Ameongeza kuwa mazingira mazuri ya mazoezi yanaendelea kuwasaidia wachezaji kurejea kwenye ubora wao kwa haraka.

Aidha, amesema benchi la ufundi linaendelea kufuatilia maendeleo ya kila mchezaji kwa karibu ili kuhakikisha timu inaingia kwenye michezo iliyobaki ikiwa kwenye hali bora zaidi.

 Kwa upande wake, Meneja wa Fountain Gate FC, Zamkufo Elias amesema timu hiyo bado inaendelea kufanya tathmini ya michezo iliyopita kwa lengo la kurekebisha makosa yaliyojitokeza kabla ya mechi zijazo.

Zamkufo amesema ushindani wa ligi kwa sasa ni mkubwa kutokana na baadhi ya timu kupigania ubingwa huku nyingine zikisaka nafasi ya kubaki salama kwenye ligi, hali inayofanya kila mchezo kuwa na ushindani mkubwa zaidi.


Kwa upande wake, mchezaji wa Fountain Gate FC, Shomari Mponzi amesema wachezaji wameendelea kushirikiana kwa karibu kuhakikisha timu inapata matokeo mazuri katika michezo iliyobaki ya ligi. Pia amewataka mashabiki kuendelea kuiunga mkono timu hiyo katika kipindi hiki muhimu huku akisisitiza kuwa kila mchezaji anaendelea kutekeleza majukumu yake kwa nidhamu na kujituma kwa ajili ya mafanikio ya klabu hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com