Mrajis msaidizi wa vyama vya ushirika Mkoa wa Shinyanga Ibrahim Kakozi akizungumza kwenye mkutano mkuu wa SHIRECU

Meneja wa Chama cha Ushirika SHIRECU Alphonce Makasi akisoma rasimu ya bajeti kwenye mkutano Mkuu wa 31
Chama Kikuu Cha Ushirika Mkoani Shinyanga (SHIRECU) kimepitisha rasimu ya bajeti ya zaidi ya shilingi bilioni 2.8 kwa mwaka wa fedha 2026/2027 huku ikijizatiti kuanza kukopesheka kwenye taasisi za kifedha.
Bajeti hiyo limepitishwa leo April 28, 2026 baada ya Meneja wa chama cha ushirika Shirecu Alphonce Makasi kuwasomea taarifa na rasimu ya bajeti kwenye mkutano Mkuu wa 31 uliowakutanisha wajumbe 202 kati ya wajumbe 214 waliokuwa wakitakiwa kuhudhuria kwenye mkutano huo.
Akisoma taarifa hiyo Meneja Makasi amesema wajumbe wakiridhia kupitishwa kwa bajeti zaidi ya shilingi bilioni 2.8 na kukopa kwenye taasisi za kifedha wataweza kutimiza adhima ya mipango ya kuendeleza biashara ya ununuzi wa mazao.
Pia mazao hayo yatakuwa Mchanganyiko,uanzishwaji na kufufua kiwanda kipya cha kukamua mafuta ya alizeti na kuendeleza duka la pembejeo.
“Awali taasisi za kifedha zilikataa kabisa kutukopesha kutokana na kuwepo kwa vikwazo vya deni kutoka benki ya Uwekezaji ya (TIB) lakini sasa tumeanza kuonyesha uaminifu wa kulipa na kupata ruhusa ya kuendelea kukopesheka kwenye taasisi za kifedha zozote nchini”amesema Makasi.
Kwa upande wake Mwenyekiti wa bodi ya Shirecu Naomi Chaba amesema kuna vyama vya ushirika (Amco’s) 107 na wanachama 7413, ambapo mpango ulioanza mwaka 2025 hadi Februari 2026 wamefanikiwa kununua mazao Mchanganyiko kama choroko na dengu,kugawa kompyuta mpakato 50 nakutoa mafunzo
"Pia ,tumefanikiwa kukarabati shule ya sekondari Buluba na kusomesha wanafunzi 28 wa kidato cha tano kwa awamu, kwa gharama ya shilingi Milioni 45." pia Chama kinatarajia kujenga kiwanda cha dengu kufanya biashara ya pamba ukarabati wa magala , amesema Chaba
Naye Mrajis msaidizi wa Ushirika mkoa wa Shinyanga Ibrahim Kakozi amesema taasisi za kifedha sasa zikae sawa kuwakopesha shirecu huku akiwataka wajumbe waeleze yale ambayo wanataka yatekelezwe na yakikwama waihoji bodi nakutoa ushauri zaidi nini kifanyike ili kuboresha zaidi.
"Niombe kila Amcos iripoti kila tatizo lililopo ili chama kiweze kufuatilia na kujua tatizo nini, kwani mkileta kwa barua itakuwa ni rahisi kufuatiliwa kwa haraka zaidi"amesema Kakozi.

Mbunge wa Jimbo la Kishapu Lucy Mayenga akizungumza kwenye mkutano wa SHIRECU


.png)




.jpg)











Social Plugin