
Na Mwandishi Wetu
Waziri Dousa alidai Tanzania "imekwama kwenye Ujamaa" na "haina maendeleo." Hapa ndipo Balozi Matinyi alipoamua kuvua glavu. Kupitia gazeti hilo hilo la Aftonbladet, Matinyi ameiambia dunia kuwa Tanzania si ile ya mwaka 1961.
Balozi Matinyi hakujibu kwa hasira, alijibu kwa hekima na namba. Aliwakumbusha Waswidi kuwa wakati wao wana vyuo vikuu 18, Tanzania sasa ina vyuo 36. Wakati wao wakidhani tunasubiri misaada yao ya SEK milioni 560 (dola milioni 60), Tanzania inakusanya zaidi ya Dola Bilioni 4 kupitia dhahabu pekee!
Huu ni ujumbe kwa dunia: Tanzania sasa inatafuta Wafanyabiashara, siyo Wafadhili. Tunajenga Reli ya Kisasa (SGR), tuna mradi wa Gesi wa Dola Bilioni 42, na uchumi wetu unakua kwa kasi kuliko wa kwao. Jibu la Matinyi si tu utetezi wa kidiplomasia, bali ni tangazo la Uhuru wa Kiuchumi.
Ni wakati wa watanzania kujivunia hatua tuliyopiga. Kama Balozi wetu alivyosema, kuitaja Tanzania kama nchi isiyo na maendeleo ni "upotoshaji wa kusikitisha." Tanzania imepaa, na aliyelala bado anadhani tuko gizani.
Social Plugin