Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

HAMZA TANDIKO AENDELEA KUWASHA MOTO WA KAMPENI... AOMBA WANANCHI WAJITOKEZE KWA WINGI 'KUTIKI' KWA WAGOMBEA WA CCM OKTOBA 29


Mgombea udiwani Kata ya Maganzo Hamza Tandiko akiwa kwenye mkutano wa kampeni katika kijiji cha Masagala akinadi sera za chama cha Mapinduzi CCM na kuwaomba wananchi wamchague Rais Samia Suluhu Hassan,Lucy Mayenga mgombea ubunge Jimbo la Kishapu na wampe kura zote za ndiyo yeye mgombea Udiwani.



Mgombea Udiwani Kata ya Maganzo Hamza Tandiko amewaomba wananchi kwenda kupiga kura Oktoba 29 ili watimize haki yao ya msingi ya kikatiba na kuwapuuza watu wanaosema hawapigi kura kwani hao hawajui haki yao wanatakiwa kuelimishwa .

Akizungumza na wakazi wa Kijiji cha Masagala Kata ya Maganzo,mgombea Udiwani amesema nchi inaamani kwani Jeshi liko imara kulinda nchi na hakuna vurugu na kuwaomba kwenda kupiga kura siku ikifika  wachague viongozi wanaotokana na chama cha Mapinduzi ili waendeleze maendeleo.

Ametumia mkutano huo kutoa elimu namna ya kupiga kura  kuanzia Rais,wabunge na madiwani huku akiwaomba kuhakikisha wanaweka tiki ya ndiyo nafasi ya udiwani ili waweze kumchagua kuwa diwani wao  kwa kumpa kura nyingi za ndiyo kwa kuwa hana mpinzani isipokuwa atapigiwa kura ya ndiyo nay a hapana.

Katibu Mwenezi wa CCM Kata ya Maganzo Juma Rajabu amesema vurugu huwa zinachanzo chake na kuwaomba wananchi wa Kata hiyo wasikubali kutumika na kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani kwa kuvunja sheria .

Amewaomba kupuuza uzushi unaotolewa kwenye mitandao ya kijamii ambao umekuwa ukisababisha hofu na kueleza kuwa kuna amani ya kutosha siku ya uchaguzi watapiga kura kwa amani na kurudi nyumbani kwa amani .

Amewaomba wazee kukaa na vijana wao kuwaonya wasijaribu kujihusisha na vurugu zozote zile ambazo zinaweza kuachilia uvunjifu wa amani ikiwa ni pamoja na kuepuka kujihusisha na maandamano yasiyo ya msingi.


Katibu Mwenezi Kata ya Maganzo Juma Rajabu akizungumza na wananchi wa Kijiji cha Masagala kwenye mkutano wa kampeni






                         













































 























Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com