Na Mwandishi wetu Malunde 1 Blog
Mshereheshaji Maarufu wa matukio mbalimbali na Mshindi wa tuzo ya MC Bora Mwanamke kinara Kanda ya ziwa Anascholastica Mathew Ndagiwe maarufu kama MC Mama Sabuni amechukua fomu kuwania nafasi ya Udiwani wa Viti Maalum kupitia chama cha Mapinduzi katika kata ya Ibadakuli manispaa ya Shinyanga kwenye uchaguzi Mkuu wa 2025.
Mc Mama Sabuni amechukua fomu hiyo mapema leo Julai 02, 2025 katika ofisi za Chama cha Mapinduzi CCM wilaya ya Shinyanga Mjini.
Social Plugin