
Semina hiyo imefanyika leo Juni 25, 2025 katika Chuo cha Ufundi Stadi (VETA)
Shinyanga kilichopo manispaa ya Shinyanga.
Akizungumza wakati wa semina hiyo, Afisa wa kodi
kutoka TRA Shinyanga Semeni Mbeshi, amesema lengo ni kuwajengea msingi mzuri wa
kizalendo vijana wanaotarajia kuingia kwenye soko la ajira na kujiajiri baada
ya kuhitimu masomo yao.
Ameongeza kuwa elimu hiyo ni endelevu na inalenga kujenga taifa la watu waaminifu
katika ulipaji wa kodi, huku akisisitiza matumizi ya Mashine za risiti za Kielektroniki (EFD) kwa wafanyabiashara na
kutoa na kudai risiti pindi wanaponunua bidhaa.
“Haki ya mlipa kodi ni kuaminiwa pindi anapofika kwenye ofisi za TRA kwa ajili
ya kufanyiwa makadirio yanayoendana na biashara yake, ni wajibu wa kila
mfanyabiashara kutoa taarifa ya ufanyaji wa biashara kwa mamlaka ya mapato TRA,
Mashine za risiti za Kielektroniki (EFD) zinasaidia kuweka rekodi sahihi ya kumbukumbu ya
biashara kwa muda wa miaka 5, lakini kodi hiyo inakwenda moja kwa moja kwenye
mfuko wa serikali na kuwezesha maendeleo kwenye taifa letu”, amesema Semeni
Mbeshi.
Kwa upande wake, Mkufunzi katika Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Shinyanga, Emili
Shirima amesema vitendo vya baadhi ya watu kutumia vishoka kujipatia huduma za
kikodi si sahihi na ni hatari kwa uchumi wa taifa, na amewataka wanachuo
kujiepusha na tabia hizo mara watakapoingia kwenye shughuli za uzalishaji mali.
Baadhi ya wanachuo walioshiriki mafunzo hayo wameishukuru TRA kwa kuwapa elimu hiyo muhimu, wakisema itawasaidia mara baada ya kuhitimu na kuanzisha biashara au shughuli za kujitegemea na kuongeza kuwa sasa wanaelewa kwamba ulipaji wa kodi unasaidia huduma za jamii kama afya, elimu na miundombinu.
Afisa wa kodi kutoka TRA Shinyanga Semeni Mbeshi akizungumza wakati wa mafunzo hayo.





















Mkufunzi katika Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) Shinyanga, Emili Shirima akizungumza mara baada ya elimu hiyo kutolewa.



Social Plugin