![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhbK95r32zVX9kezUrQZVVlhRTT99kxQG5Ls3eHwuZXVWJhMta9o33bMtFVw-UHotjWT9O_C0ZUDKa9pMToIWsGw1vEq6_Pm9xZkCC3_Ljgfc9dcRMiH85YSbShe1G_6wI2X7Z4GF4TlnI0Xk4WQjCl7PwPLAt48OR8hJ43bP4i0RenEWOqnD2BDyUj/w640-h426/IMG-20240502-WA0092.jpg)
Waziri wa Kilimo, Mhe. Hussein Bashe (Mb) akiwasilisha Hotuba ya Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Fedha ya Wizara ya Kilimo kwa Mwaka 2024/2025 amesema kuwa uzalishaji wa chakula kwa msimu wa kilimo wa 2022/2023 ulitosheleza mahitaji ya chakula ya tani 16,390,404 kwa mwaka 2023/2024 na kuwepo kwa ziada ya tani 4,011,611.
Amesema kutokana na hali hiyo, Taifa limejitosheleza kwa chakula kwa asilimia 124 ikilinganishwa na utoshelevu wa asilimia 114 mwaka 2022/2023. Aidha, utoshelevu wa chakula unatarajiwa kufikia asilimia 130 ifikapo mwaka 2025