TIGO YAKUTANA NA WADAU WAKE KWENYE JUKWAA LA WAFANYABIASHARA NA WAJASIRIAMALI SHINYANGA


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Kampuni ya TIGO Tanzania imekutana na wadau wake Mkoa wa Shinyanga katika Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali lenye lengo la kutoa fursa kwa wafanyabiashara kujua huduma na bidhaa za Kibiashara, Kifedha na za dukani zilizoambatana na uboreshaji wa mtandao wa 4G+ kimkoa na Kanda ya ziwa kwa ujumla.

Akizungumza wakati wa Jukwaa hilo lililofanyika Ijumaa Mei 10,2024 usiku katika ukumbi wa Karena Hotel Mjini Shinyanga, Mkurugenzi wa Kampuni ya TIGO Tanzania Kanda ya Ziwa, Joseph Mutalemwa amesema TIGO imeendelea kuboresha huduma za kuingiza sokoni bidhaa mpya hivyo kuwaomba wadau kuchangamkia fursa zinazopatikana katika Kampuni hiyo.

Amesema Kampuni  ya TIGO imetoa elimu ya bidhaa na  huduma  zake zinazorahisisha biashara kwa taasisi mbalimbali ili kuweza kukuza biashara zao na kuongeza wateja.

"Tumekutana na wadau wetu wakiwemo wafanyabiashara na wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga ili kuwaeleza na kuwatambulisha bidhaa zetu pamoja na huduma zetu zikiwemo za Mobile solutions, APN, Bulk sms, E1, Toll-free, Mjasiriamali box, 5G standalone, Collection account, Disbursement account, Huduma za kikoba, Lipa kwa Simu, Huduma simu za mkopo, Huduma za kurudisha number (simswap) na Huduma za kuoanisha number (special number)",ameeleza Mutalemwa.
Mkurugenzi wa Kampuni ya TIGO Tanzania Kanda ya Ziwa, Joseph Mutalemwa akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania. Picha na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Mkurugenzi wa Kampuni ya TIGO Tanzania Kanda ya Ziwa, Joseph Mutalemwa akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Meneja wa Kampuni ya TIGO Mkoa wa Shinyanga Sadock Mahundo akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Meneja wa Kampuni ya TIGO Mkoa wa Shinyanga Sadock Mahundo akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Meneja wa Kampuni ya TIGO Mkoa wa Shinyanga Sadock Mahundo akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Meneja wa Mauzo  Taasisi Ndogo na Kati wa Kampuni ya TIGO Kanda ya Ziwa, Paschal Mathew akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Meneja wa Mauzo Mashirika na Taasisi Kubwa wa Kampuni ya TIGO Kassongo Faraji akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Meneja wa Kampuni ya TIGO Tanzania Kanda ya Ziwa, Christopher Charles akizungumza wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Msimamizi wa Duka Kampuni ya TIGO Mkoa wa Shinyanga, Pendo Ally akieleza kuhusu Simu za mkopo zinazouzwa katika duka hilo wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Msimamizi wa Duka Kampuni ya TIGO Mkoa wa Shinyanga, Pendo Ally akieleza kuhusu Simu za mkopo zinazouzwa katika duka hilo wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania
Msimamizi wa Duka Kampuni ya TIGO Mkoa wa Shinyanga, Pendo Ally akieleza kuhusu Simu za mkopo zinazouzwa katika duka hilo wakati wa Jukwaa la Wafanyabiashara na Wajasiriamali Mkoa wa Shinyanga lililoandaliwa na Kampuni ya TIGO Tanzania



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post