MR. MANGURUWE AGAWA TIKETI BURE KWA MASHABIKI, WASHUHUDIE MCHEZO WA SIMBA SC Vs DODOMA JIJI

Mkurugenzi wa Kampuni ya Kijiji cha Nguruwe Project kilichopo Zamahero wilaya ya Bahi Mkoani Dodoma Simon Mnkondya maarufu Mr Manguruwe amegawa bure tiketi 100 kwa Mashabiki wa Soka kwa ajili ya kushuhudia mchezo kati ya Simba SC na Dodoma Jiji utakaofanyika kesho Ijumaa Mei 17,2024 katika uwanja wa Jamhuri Dodoma.

Mr Manguruwe ambaye ni shabiki kindakindaki wa Timu ya Simba SC amegawa tiketi hizo leo katika soko la Machinga Complex Dodoma.

"Katika kuunga mkono juhudi za serikali katika kuinua michezo nchini kama ilivyo kwa Rais wa serikali ya Jamhuri ya mlmuungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye amekuwa akinunua magoli katika vilabu vya Simba SC na Yanga leo hii nimegawa tiketi 100 kwa mashabiki kuelekea mechi ya Dodoma Jiji dhidi ya Simba SC mchezo utakaopigwa katika uwanja vya Jamhuri Dodoma", amesema Tajiri huyo wa Nguruwe maarufu Mr Manguruwe.

Wasiliana na Mr Manguruwe kwa simu namba Namba +255763755755

Tazama Video HAPA



Soma pia 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post