BASHE KUONGOZA MKUTANO WA WADAU WA TASNIA YA MBEGU LEO DODOMA

 


Na Nyabaganga Taraba - Dodoma

Mkutano Mkuu wa wadau wa Tasnia ya mbegu  Tanzania unafanyikaleo Jijini Dodoma ambapo mgeni  rasmi ni Waziri wa Kilimo Mhe Hussein Bashe.

 Miongoni mwa mada zitakazowasilishwa kwenye mkutano huo wadau wa Tasnia ya mbegu ni Hali ya Tasnia ya mbegu na mpango wa uendelezaji mbegu, Majukumu ya SAGCOT katika kuwezrsha upatikanaji wa mbegu za mazao  ya biashara na viazimviringo na Mikakati ya kuwezrsha upatikanaji wa mbegu za awali za mazao mbalimbali.

Mada zingine ni fursa za biashara ya mbegu Bora'' za mazao ya Kilimo , uthibiti wa ubora wa mbegu,fursa za ajira za wanawake na vijana kupitia Tasnia ya mbegu, upatikanaji wa mbegu Bora'' za mazao ya mbogamboga na Miche Bora'' ya miti ya matumda na mada  ya kujengea uwezo  wazalishaji mbegu kupitia BBT.

Baada ya Majadiliano wadau hao watatoka na maazimio ya pamoja  lengo likiwa yale watakayokubaliana yatatekelezwa.

Aidha maonesho ya wadau wa mbegu yapo katika eneo la viwanja  vya Hotel ya Morena Jijini Dodoma.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post