MJUMBE wa Baraza Kuu la Jumuiya ya Umoja wa Wanawake Tanzania(UWT)Taifa na Mjumbe wa Kamati ya Utekelezaji wa jumuiya hiyo Marima Ulega amekabidhi simu za mkononi tisa kwa ajili ya kufanikisha usajili wanachama kieletroniki ndani ya Mkoa wa Pwani.
Akizungumza na wana UWT Mkoa wa Pwani wakati wa hafla ya kukabidhi simu hizo Mariam Ulega amesema kwa sasa wanaona na wanaendelea kujivunia matunda ya uongozi wa Rais Dk.Samia Suluhu Hassan na hakika amekuwa mwananmke shupavu na mwenye mapenzi makubwa na wanawake wa Tanzania hasa UWT.

“Sisi wana UWT tufanye kazi na tupite kwa wananchi tukielezea mazuri yaliyofanywa na Rais.Hatuwezi kufanikiwa kama hatuna ongezeko la wana chama hivyo tunatakiwa tuwavute wanachama wapya , tusajili wanachama wapya kieletroniki na hiyo itatusaidia.
.jpeg)
Amefafanua kuna mtandao wa UWT ambao umeanzishwa unaosajili wanachama keletroniki na Mkoa wa Pwani kuna wilaya moja ndjo inaonekana inasajili wanachama.Hata hivyo kunachangamoto ya vitendea kazi.
.jpeg)
“Makatibu wa UWT naaawamini hivyo tuhakikishe tunahamasisha wanachama wapya kwa kuwasijili sambamba na kuwaelezea UWT ni nini na inafanya kazi zipi na iwapo watajiunga nayo watapata faida zipi.
“Mwenyekiti wetu wa UWT Taifa tunamuona anahimiza usajili, tukiwa na wanachama wengi tutasonga mbele hivyo simu janja ninazokabidhi zinakwenda kurahisisha shughuli za usajili.”
.jpeg)
.jpeg)
Social Plugin